Kutoboa mwili kumekua kitu maarufu siku za karibuni na imekua kama njia ya kujielezea na kujitambulisha. Kutoboa midomo kunaweza kuonekana ni kitu kizuri na cha kupendeza lakini kinaweza kuleta madhara makubwa kwa mwili na afya. Hii ni kwa sababu kinywa kina vijududu vingi sana ambavyo vinaweza kusababisha maambukizi na kuvimba hasa baada ya kutoboa sehemu za kinywa na midomo. Kama umetoboa ulimi, mashavu, midomo (lips) na kilimi (sehemu ya nyuma kabisa ya koo), hii inaathiri sana kuongea, kutafuna na pia kumeza, vilevile inaweza ikasababisha; Maambukizi, maumivu na kuvimba. Kwa sababu ya uwingi wa bakteria katika kinywa, kutoboa sehemu za kinywa kunaweza sababisha maambukizi ambayo huwa pamoja na maumivu na kuvimba. Kuvimba kwa ulimi au sehemu aya nyuma ya koo kunaweza sababisha kukosa pumzi na hata kupoteza maisha. Kuharibika kwa meno na fizi Mzio au Allergy Kuharibika kwa mishipa ya fahamu. Hii ni hasa kwa kutoboa ulimi. kunaweza kusababisha kuharibika kwa miship...