TATIZO LA KUKOSA PUMZI NA KUKOROMA WAKATI WA KULALA
Kukosa pumzi wakati wa kulala (sleep apnea) ni tatizo ambalo hutokea wakati upumuaji wa kawaida huingiliwa wakati mtu akiwa usingizini. Kukoroma ni tatizo linalowapata watu wengi wanaopata shida ya ya kupumua wakati wakiwa usingizini ila sio wote wanaokoroma wanapata shida ya kupumua.
Kuna aina mbili za kukosa pumzi wakati wa usingizi;
- Obstructive sleep apnea. Hii ndio ya kawaida na inawapata watu wengi. Hutokea pale njia ya hewa inapokua imezibwa wakati wa usingizi. Matatizo ya kiafya kama uzito uliopitiliza huchangia sana kwenye hili.
- Central sleep apnea. Hii hutokea pale ambapo ubongo unashindwa kupeleka taarifa na kuamsha misuli ya upumuaji. Njia za hewa zinakua wazi ila ubongo hushindwa kuamsha misuli. Hii huwapata sana watu waliopooza, wenye saratani ya ubongo na moyo kushindwa kufanya kazi(heart failure).
- Umri zaidi ya miaka 40
- Uzito mkubwa/uliopitiliza
- Historia ya ugonjwa kwenye familia
- Kuziba kwa pua kutokana na mzio (allergies)
- Kuwa na ulimi mkubwa na taya ndogo
- Kubadilisha jinsi ya kulala. kuacha kulala kwa mgongo.
- Vifaa vya kinywa. Vifaa mbalimbali vya mdomo vinaweza kusaidia katika kupunguza tatizo hili la kukosa pumzi. madaktari wa kinywa na meno wanaweza kusaidia katika matibabu yake
- Upasuaji
![]() |
| Kifaa cha kuzuia tatizo la kukosa pumzi |
KAMA UNA TATIZO LA KUKOSA PUMZI USINGIZINI AU KUKOROMA HAKIKISHA UNAONANA NA DAKTARI AU DAKTARI WA MENO KWA AJILI YA KUPANGA MATIBABU NA SULUHISHO SAHIHI.


Comments
Post a Comment