Kutoboa mwili kumekua kitu maarufu siku za karibuni na imekua kama njia ya kujielezea na kujitambulisha. Kutoboa midomo kunaweza kuonekana ni kitu kizuri na cha kupendeza lakini kinaweza kuleta madhara makubwa kwa mwili na afya. Hii ni kwa sababu kinywa kina vijududu vingi sana ambavyo vinaweza kusababisha maambukizi na kuvimba hasa baada ya kutoboa sehemu za kinywa na midomo.
Kama umetoboa ulimi, mashavu, midomo (lips) na kilimi (sehemu ya nyuma kabisa ya koo), hii inaathiri sana kuongea, kutafuna na pia kumeza, vilevile inaweza ikasababisha;
- Maambukizi, maumivu na kuvimba. Kwa sababu ya uwingi wa bakteria katika kinywa, kutoboa sehemu za kinywa kunaweza sababisha maambukizi ambayo huwa pamoja na maumivu na kuvimba. Kuvimba kwa ulimi au sehemu aya nyuma ya koo kunaweza sababisha kukosa pumzi na hata kupoteza maisha.
- Kuharibika kwa meno na fizi
- Mzio au Allergy
- Kuharibika kwa mishipa ya fahamu. Hii ni hasa kwa kutoboa ulimi. kunaweza kusababisha kuharibika kwa mishipa ya fahamu ya ulimi na hii hupelekea athari ya mlango wa fahamu wa ladha.
- Kutokwa kwa mate mengi
- Ugumu katika matibabu ya kinywa na meno hasa linapofika suala la mionzi wakati wa kuchukua picha za xray
- Saratani ya kinywa
- Muone daktariwa meno pindi tu unapoona dalili za maumivu, uvimbe sehemu uliyotoboa
- Hakikisha unaiweka sehemu uliyotoboa safi kwa kusukutua na dawa ya kusukutua kila baada ya kula.
- Angalia kama chuma kilichowekwa sehemu uliyotoboa kimekaza kuepuka kumeza
- Toa chuma wakati wa mazoezi
- Muone daktari wa kinywa na meno mara kwa mara na hakikisha unasafisha kinywa mara mbili kwa siku
NJIA PEKEE YA KUEPUKA MATATIZO HAYA NI KUTOTOBOA KINYWA AU KUTOA VYUMA KABLA HAIJAKULETEA MATATIZO. KUTOBOA KINYWA HULETA MAJUKUMUA MAPYA KWENYE MAISHA KWA SABABU KUNAHITAJI UANGALIZI WA HALI YA JUU. USITOBOE KINYWA, ONGEA NA DAKTARI WA KINYWA NA MENO KWA USHAURI ZAIDI.
Comments
Post a Comment