MATUMIZI YA ANTIBIOTICS KATIKA AFYA YA KINYWA NA MENO
Antibiotics hutolewa pale ambapo kuna maambukizi au ugonjwa unaosababishwa na bakteria. Linapofika suala la maumivu ya jino, antibiotics zinatakiwa kuepukwa isipokua pale ambapo kuna uhitaji sana wa kuzitumia.
Kuwa na uelewa kuhusu antibiotics kutasaidia kuweza kuelezea vizuri jinsi ambavyo unajisikia kwa daktari wa meno na kupata jinsi ya kutatua tatizo. Kwa kujua dalili za maumivu ya jino daktari anaweza kujua ni matibabu gani yanafaa kulingana na tatizo. ni Daktari pekee ndiye anayejua ni wakati gani unafaa kutumia antibiotics na upi haufai kulingana na tatizo na maumivu.
Antibiotics hutolewa mara nyingi kwa maambukizi au infection ambayo imesambaa na hii huweza kutambulika kama daktari akishakuona na kutambua ukubwa wa tatizo.
Dawa ni za kipekee.
Hatuwezi kushiriki kutumia mswaki mmoja si ndivyo? Basi ndivyo ilivyo kwenye madawa, dawa inayomsaidia mtu mmoja inaweza isifanye kazi kwa mtu mwingine. Dawa zinazosaidia kutibu mafua au ugonjwa mwingine zinaweza zisisaidie kutibu matatizo ya meno na muda mwingine kupelekea kupata athari. Daktari wa meno anajua ni dawa ipi itakayokufaa kwa tatizo lako.
Athari za Kutumia Antibiotics mara kwa mara:
Matumizi yaliyopitiliza ya antibiotics husababisha ugumu katika kutibu maambukizi yanayosababishwa na bakteria (antibiotic resistant bacteria). Tumia antibiotics pale tu unapoandikiwa na daktari, hii itasaidia kufanya dawa ziwe na nguvu pale zinapotumika.
SIO KILA MAUMIVU YA JINO YANATIBIWA NA ANTIBIOTICS. USITUMIE ANTIBIOTICS BILA USHAURI NA MAELEKEZO YA DAKTARI, UKIWA NA MAUMIVU YA JINO NI VYEMA KUMUONA DAKTARI WA MENO KWA AJILI YA MATIBABU SAHIHI.
Comments
Post a Comment