Skip to main content

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO; JAMBO AMBALO KILA MWANAMKE ANAFAA KULIFAHAMU


                        Grandmother, Mother and Granddaughter


Uzito, mhemko (mood) na afya ya kinywa na meno. Kuna kitu kimoja ambacho kinaendesha hivi vitu vyote, nacho ni homoni.

Unaweza ukajiuliza ni vipi homoni zinauhusiano na afya ya kinywa na meno kwa mwanamke, hii ndio sababu; Homoni nyingi za kike (estrogen na progesterone) zikiwa katika kiwango kikubwa husababisha kuongezeka kwa mtiririko wa damu katika fizi, hii husababisha fizi kuwa sensitive na kuovereact kwa kitu chochote kinachoweza kuziirritate. Wanawake huwa ni sensitive kwa utando unaokua kwenye meno hasa wakati kiwango cha homoni zao kipo juu. Hali hiyo hupelekea fizi kuvimba na kuanza kutoa damu, hali hii isipotibiwa hupelekea ugonjwa kushika kasi na kuharibu mfupa unaoshikilia meno na kupeleka meno kulegea na kutoka.

Homoni za mwili ni maisha ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibiwa katika hatua za mwanzo kabisa. Nini hasa mwanamke anatakiwa kufanya? Anza kuzingatia na kuhakikisha afya ya kinywa na meno inakua nzuri katika vipindi hivi vitano vya maisha.

Kipindi Cha Balehe
 Girl Beautiful | Free Stock Photo | A beautiful African American ...


Kipindi hiki huwa kuna mabadiliko ya homoni ambayo huweza kupelekea msichana kuanza kupata uvimbe, wekundu na kuvuja damu kwenye fizi. Tiba mbadala ni kuhakisha unapiga mswaki mara mbili kwa siku kwa kutumia dawa ya meno yenye madini ya flouride kuhakikisha hakuna utando unabaki kwenye meno.

Kipindi Cha Hedhi.


Menstruation: Period, Psychological & Cultural Consideration ...
Mara nyingi huwa kuna mabadiliko ya hali ya kinywa siku chache kabla ya hedhi na wakati wahedhi ikiendelea. Mabadiliko hayo ni pamoja na fizi kuvimba, kuvuja damu na kutokea kwa vidonda mdomoni. Yote hayo husababishwa na mabadiliko ya homoni. Hali hii huisha punde tu hedhi inapokwisha, ila tunashauri sana kufanya usafi wa kinywa mara dufu katika kipindi hiki ili kuzuia magonjwa ya fizi. na kwasababu hedhi ni kila mwezi, inaweza kufanya tatizo la fizi likawa kubwa zaidi.

Kipindi cha Matumizi ya dawa za kuzuia Mimba.
Once-a-month oral contraceptive pill in tests - BBC News
Moja ya athari za matumizi ya dawa za kuzuia mimba ni kuvimba na kuvuja damu kwa fizi. Ingawa dawa za sasa wamepunguza kiwango cha homoni hizi ila ni muhimu kujua athari zake kwa afya ya kinywa na meno. Tunashauri kwa anayetumia hizi dawa afanye uchunguzi wa kinywa mara kwa mara na pia usafi wa kinywa uzingatiwe.

Kipindi Cha Ujauzito.

 Heavily Pregnant Woman Shot in Abdomen in Michigan Parking Lot ...
Kipindi cha ujauzito ni kipindi ambacho wanawake wengi hupata matatizo ya meno na fizi. Moja ya hali inayotokea kipindi hiki ni kuvimba kwa fizi. Tunashauri, kwa kina mama wote wajawazito, kuhakikisha wanafanya usafi wa kinywa mara dufu na pia kufanya uchunguzi na usafi wa kinywa kwa daktari wa meno mara kwa mara.

Kipindi cha kuisha kwa vipindi vya hedhi (menopause)

 African Old Woman Images, Stock Photos & Vectors | Shutterstock
Menopause ni mabadiliko makubwa sana kwa maisha ya mwanamke. Kipindi hiki mwanamke huwa anapata mabadiliko katika ladha ya ulimi, kukauka kwa mdomo, ganzi na zaidi ya yote ni kupoteza sehemu za mifupa. Hii yote husababishwa na mabadiliko ya homoni. Ukavu wa mdomo husababisha mzunguko wa mate kupungua mdomoni na hii hupelekea kuwepo kwa nafasi ya meno kutoboka kwa urahisi. Unachokula kinaweza kufanya mabadiliko hasa inapofika suala la mdomo mkavu. Epuka kula vitu vyenye sukari, chumvi na pilipili kwa wingi. Epuka pombe, sigara na vinywaji vyenye caffein hivi hufanya hali ya mdomo mkavu izidi kuwa mbaya zaidi.

MABADILIKO YA HOMONI KWENYE MWILI YANA ATHARI KUBWA KWA AFYA YA KINYWA NA MENO KWA MWANAMKE. ZINGATIA KILA KIPINDI CHA MAISHA NA CHUKUA HATUA STAHIKI KUHAKIKISHA AFYA YA KINYWA NA MENO INAKUA NZURI NA IMARA

Comments

Popular posts from this blog

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika. Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea. Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako. 1. Balehe Mabadiliko ya...

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025

 

PLASTIC FREE SMILES PROJECT 2023-2024

  Plastic Free Smiles project is an environmental and oral health project designed by Dr. Winfred Mgaya under the umbrella of Tanzania Oral Health Foundation. The project aims to raise awareness on the effects of plastic pollution to the environment specifically caused by plastic toothbrushes and advocating on the adoption of eco-friendly toothbrushes to reduce the plastic pollution caused by plastic toothbrushes. The project is structured to have two phases that will start from November 2023 to April 2024 and May 2024 to November 2024. The project includes physical meetings with target groups as well as online and social media campaigns OBJECTIVES The objective of the advocacy campaign is to raise awareness of the environmental impact of plastic toothbrushes while encouraging people to make the switch to eco-friendly toothbrushes. Specifically, the objectives are: 1. To educate the public on the harmful effects of plastic toothbrushes on the environment. 2. To promote t...