Skip to main content

MATIBABU YA KUSAFISHA MIZIZI YA MENO (ROOT CANAL)




 Root Canal Treatment to Save Your Teeth • West Cobb Dentistry📲770 ...






Kama una jino lililoharibika sana, kuoza au lenye maambukizi (infection), daktari wa meno anaweza akashauri matibabu ya kusafisha mizizi au root canal. Matibabu ya kusafisha mizizi ya jino yanatumika kuokoa jino pale inapohitajika badala ya kulitoa.

Nini Hufanyika katika matibabu ya kusafisha mizizi ya jino?


Root Canal Treatment in Drouin | Bank Place Dental
Jinsi jino lilivyo kwa muonekano wa ndani.


Jino huwa na nafasi ndani yake ambayo huwa na mishipa ya fahamu na damu ambayo hulifanya jino liwe hai. Sehemu hii inaweza kupata maambukizi kama;
  • Una tundu kwenye jino ambalo ni kubwa sana
  • Matibabu ya muda mrefu ambayo yanaweza kusababisha matatizo kwa sehemu hii.
  • Jino likivunjika au kupasuka
  • Ajali yoyote kwenye jino
Ukiwa na moja ya matatizo hayo na yasitibiwe, jino hupata maambukizi na kusababisha maumivu makali na wakati mwingine uvimbe ambao husababishwa na jipu linaloota kwenye ncha ya mzizi wa jino. Maambukizi haya yanaweza kusababisha kupoteza jino kwa sababu bacteria wanaosababisha maambukizi hayo wanaweza kuharibu mfupa unaoshikilia jino katika taya.

Nini ha kutegemea wakati wa matibabu haya?

Matibabu ya kusafisha mizizi huweza kuchukua awamu mbili mpaka tatu ili kumalizika. Huwa ni matibabu ambayo hayana maumivu kwa sababu daktari hutumia ganzi wakati wa matibabu na mwisho wa matibabu maumivu uliyokuwa nayo mwanzoni yanatakiwa kuwa yamekwisha kabisa.

Kabla ya matibabu daktari atafanya yafuatayo;
  • Atapiga picha ya x ray ili kuangalia jino na mfupa unaolizunguka
  • Atakuweka ganzi ili kuondoa maumivu na kukufanya uwe mtulivu na vizuri wakati wa matibabu
Wakati wa matibabu daktari atafanya yafuatayo;
  • Atatengeneza uwazi juu ya jino ili kuifikia sehemu yenye mishipa ya damu na fahamu.
  • Atatoa mishipa ya damu na fahamu na damu kutoka kwenye jino na sehemu ya mizizi ambayo hufahamika kama mifereji au canals
  • Atasafisha mifereji ya mizizi kwa kutumia dawa ambazo husaidia kuondoa vijidudu vilivyopo humo.
  • Mwisho wa matibabu mifereji ya mizizi huzibwa ili kuzuia kitu chochote kisiingie kwenye jino, na pia jino huzibwa tayari kwa kuendelea na matumizi yake. Kama jino limeharibika sana wakati mwingine linaweza kuhitaji kuwekewa kofia au crow ni vizn ambayo huifanya jino liwe imara zaidi.
Baada ya matibabu unaweza kuhisi maumivu madogo saaana ambayo hupotea baada ya siku kadhaa ni vizuri kumtaarifu daktari kwa kitu chochote unachoweza kuwa unahisi.

Jino lililozibwa baada ya Matibabu ya kusafisha mizizi hukaa kwa muda gani?

Likiwa linasafishwa vizuri jino hukaa kwa maisha yote. Muhimu ni kusafisha meno vizuri kwa dawa yenye madini ya flouride, kusafisha katikati ya meno kwa uzi maalumu au floss, na pia kumuona daktari wa meno mara kwa mara ili kuhakikisha meno yanabaki kuwa na afya na imara.

Comments

Popular posts from this blog

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika. Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea. Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako. 1. Balehe Mabadiliko ya...

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025

 

PLASTIC FREE SMILES PROJECT 2023-2024

  Plastic Free Smiles project is an environmental and oral health project designed by Dr. Winfred Mgaya under the umbrella of Tanzania Oral Health Foundation. The project aims to raise awareness on the effects of plastic pollution to the environment specifically caused by plastic toothbrushes and advocating on the adoption of eco-friendly toothbrushes to reduce the plastic pollution caused by plastic toothbrushes. The project is structured to have two phases that will start from November 2023 to April 2024 and May 2024 to November 2024. The project includes physical meetings with target groups as well as online and social media campaigns OBJECTIVES The objective of the advocacy campaign is to raise awareness of the environmental impact of plastic toothbrushes while encouraging people to make the switch to eco-friendly toothbrushes. Specifically, the objectives are: 1. To educate the public on the harmful effects of plastic toothbrushes on the environment. 2. To promote t...