Skip to main content

AFYA YA KINYWA NA MENO KWA WAJAWAZITO

AFYA YA KINYWA NA MENO KWA WAJAWAZITO

Image result for pregnancy and oral health

Ujauzito ni kipindi ambacho mwanamke anakua ana mahitaji mengi na mabadiliko mengi katika mwili na baadhi ya mabadiliko hayo yana athari kwa afya ya kinywa na meno kama hakutakua na uangalizi mzuri wa kinywa na meno kwa kipindi cha ujauzito.

Moja ya matatizo ya kinywa na meno yanayowapata wajawazito wengi ni tatizo la fizi kuvimba na kutoa damu ambayo kitaalamu inaitwa "pregnancy gingivitis au pregnancy tumour".
Tatizo hili husababishwa na kuongezeka kwa kiwango cha homoni iitwayo "progesterone" ambayo huchangia kuongezeka kwa mtirirko wa damu kwenye fizi na kuzifanya ziwe sensitive, kuvimba na rahisi kutoa damu wakati wa kupiga mswaki. Mabadiliko ya kiwango cha homoni hii pia huwapa urahisi bakteria ambao husababisha magonjwa ya fizi kukua na kusababisha magonjwa ya fizi.
Tatizo hili la fizi linaweza kutokea muda wowote kuanzia mwezi wa pili mpaka wa nane lakini huwa kwa kasi sana katika kipindi cha pili cha ujauzito (second trimester) kuanzia mwezi wa tatu mpaka wa sita.

Image result for pregnancy gingivitis
Pregnancy gingivitis

Kuna umuhimu gani wa kutibu magonjwa ya fizi kwa wajawazito?

Matibabu ya magonjwa ya fizi kwa wajawazito ni muhimu sana kabla hayajakua na kufikia hali mbaya ambayo inaweza kupelekea meno kutoka au kutolewa. Afya ya mama mjamzito na afya ya mtoto inaweza kuathiriwa kwa kiwango kikubwa na afya ya kinywa na meno hasa tatizo hili la fizi kwa sababu wakati huu mama mjamzito huwa anapata tabu sana kwenye kula hii hupelekea afya yake kuzorota na ya mtoto pia. Tafiti nyingi zinaonesha kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya matatizo ya fizi na meno na kuzaliwa kwa watoto njiti (premature delivery).

Nini kifanyike ili kuepuka matatizo ya fizi wakati wa ujauzito?

Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia ili kuhakikisha una afya nzuri ya kinywa na meno kwa kipindi chote cha ujauzito.
  • Hakikisha unamuona daktari wa meno mara kwa mara ili kuhakikisha hakuna tatizo lolote la meno na kama lipo basi linashughulikiwa mapema iwezekanavyo.
  • Tumia mswaki wenye brush laini  na kupiga mswaki taratibu ili kuepusha kuziumiza fizi ambazo kwa wakati huo zinaweza kutoa damu kwa urahisi.
  • Tumia dawa ya meno yenye madini ya flouride kwa kupiga mswaki mara mbili kwa siku
  • Hakikisha unasukutua mdomo kwa dawa ya kusukutua na pia kila unapopata hali ya kutapika ili kuepusha tindikali itokayo tumboni kubaki kwenye meno na kusababisha meno kutoboka.
  • Kula chakula bora chenye uwingi wa madini ya calcium na phosphorus, protini na vitamini A C na D.
AFYA YA KINYWA NA MENO KWA MAMA MJAMZITO NI MUHIMU KWA AFYA YAKE NA AFYA YA MTOTO PIA.

Comments

Popular posts from this blog

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika. Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea. Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako. 1. Balehe Mabadiliko ya...

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025

 

PLASTIC FREE SMILES PROJECT 2023-2024

  Plastic Free Smiles project is an environmental and oral health project designed by Dr. Winfred Mgaya under the umbrella of Tanzania Oral Health Foundation. The project aims to raise awareness on the effects of plastic pollution to the environment specifically caused by plastic toothbrushes and advocating on the adoption of eco-friendly toothbrushes to reduce the plastic pollution caused by plastic toothbrushes. The project is structured to have two phases that will start from November 2023 to April 2024 and May 2024 to November 2024. The project includes physical meetings with target groups as well as online and social media campaigns OBJECTIVES The objective of the advocacy campaign is to raise awareness of the environmental impact of plastic toothbrushes while encouraging people to make the switch to eco-friendly toothbrushes. Specifically, the objectives are: 1. To educate the public on the harmful effects of plastic toothbrushes on the environment. 2. To promote t...