NJIA ZA KUSAIDIA KUACHA UVUTAJI WA SIGARA NA MATUMIZI YA TUMBAKU
Tunafahamu kuwa uvutaji wa sigara na matumizi ya tumbaku ni hatari kwa afya, hivyo basi haitakua kitu kigeni kufahamu kuwa matumizi ya sigara na tumbaku yana athari kwa afya ya kinywa na meno pia. Matumizi ya sigara na tumbaku husababisha harufu mbaya ya kinywa, lakini huo ni mwanzo tu wa athari hizo. Matumizi ya sigara na tumbaku husababisha;
- meno na ulimi kupata rangi nyeusi au "stains"
- vidonda vya midomoni kutopona kwa haraka hasa baada ya meno kutolewa
- Magonjwa ya fizi
- Saratani ya kinywa
- Kuwa na lengo. Ukiamua kuacha matumizi ya sigara na tumbaku, weka lengo na weka tarehe ambayo utaanza taratibu za kuacha matumizi ya sigara na tumbaku na onana na daktari wa meno kwa ushauri na msaada katika mchakato huo.
- Usifanye peke yako. Ni rahisi kuacha matumizi ya sigara na tumbaku kama ukipata msaada kutoka kwa marafiki na familia. Omba msaada wao na uwaambie wapi wanaweza kusaidia, tumia muda mwingi na watu wanaopenda ufanikiwe katika lengo lako na zungumza na watu walioweza kuacha matumizi ya sigara na tumbaku wakupe ushauri na uzoefu wao katika mchakato huo.
- Usikae bila kazi. Weka mbadala wa tabia ya uvutaji wa sigara kwa kufanya mazoezi na mambo mengine ambayo hayahusishi marafiki na watumiaji wa sigara pia tumia bubble gums zisizo na sukari kuuweka mdogo busy hii inasaidia pia kupunguza meno kutoboka.
- Epuka vitu vinavyopelekea utumie sigarana tumbaku. Epuka marafiki wanaotumia sigara, matumizi ya pombe, kahawa, msongo wa mawazo, tupa vitu vinavyotumika wakati wa kuvuta sigara, tembele sehemu ambazo uvutaji wa sigara hauruhusiwi.
- Jipongeze. Kuacha matumizi ya sigara na tumbaku sio kitu rahisi, kila saa, siku wiki ambayo inapita bila matumizi ya sigara au tumbaku inahitaji pongezi. Kwa kila pesa unayoitunza kwa kutotumia sigara unaweza jipongeza kwa kula vizuri.
MATUMIZI YA SIGARA NA TUMBAKU NI HATARI KWA AFYA YA KINYWA NA MENO NA AFYA YA MWILI KWA UJUMLA. KUACHA MATUMIZI HAYO KUTASAIDIA KUPUNGUZA ATHARI HIZO.
KUACHA MATUMIZI YA SIGARA NA TUMBAKU INAWEZEKANA, WEKA LENGO NA ANZA SASA.
Comments
Post a Comment