Skip to main content

UMRI NA AFYA YA KINYWA NA MENO

UMRI NA AFYA YA KINYWA NA MENO
Image result for old people smiling

Umri ukiwa unaongezeka inakua ni muhimu zaidi kuwa muangalifu na afya ya kinywa na meno. Kuna imani potofu kuwa kadiri mtu anavyozeeka ndivyo anavyopoteza meno yake, SI KWELI.  Kama unapiga mswaki vizuri na kuwa muangalifu na afya ya kinywa na meno, meno yako yanaweza kubaki maisha yako yote.

Kinywa hubadilika umri ukiwa unaongezeka, mishipa ya fahamu kwenye meno hubadilika na kuwa midogo zaidi na kukufanya kutohisi sana maumivu pale meno yanapotoboka. Kama utakua hufanyi check up ya meno mara kwa mara, hii hufanya matatizo yagundulike yakiwa katika hatua mbaya ambayo mara nyingine inaweza ikashindikana kutibiwa na kupeleke kupoteza meno.

Kama unataka kujisikia vizuri, kuwa na fya na muonekano mzuri, utashangazwa na jinsi kinywa chenye afya kinaweza kukubadilisha. Vifuatavyo ni vidokezo vinavyoweza kukusaidia kudumisha na kuboresha afya ya kinywa na meno kwa maisha yako yote.
  • Piga mswaki angalau mara mbili kwa siku kwa mswaki laini na dawa ya meno yenye madini ya flouridi.
  • Safisha meno katika nafasi ya jino na jino kwa kutumia floss angalau mara moja kwa siku.
  • Kama unatumia meno bandia, hakikisha unasafisha meno hayo na kuvua angalau kwa msaa nane kwa siku.
  • Kunywa maji yenye madini ya flouridi mara kwa mara
  • Kama unatumia sigara basi fanya mipango ya kupunguza na kuacha kabisa
  • Muone daktari wa meno mara kwa mara angalau mara mbili kwa mwaka (kila baada ya miezi sita)
Kwa kufuata maelekezo haya na kuwa na machaguo sahihi ya vyakula na staili za maisha, na kumuona daktari wa meno mara kwa mara kutafanya uwe na tabasamu zuri kwa kuwa na meno yenye afya kwa maisha yako yote.

Comments

Popular posts from this blog

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika. Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea. Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako. 1. Balehe Mabadiliko ya...

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025

 

PLASTIC FREE SMILES PROJECT 2023-2024

  Plastic Free Smiles project is an environmental and oral health project designed by Dr. Winfred Mgaya under the umbrella of Tanzania Oral Health Foundation. The project aims to raise awareness on the effects of plastic pollution to the environment specifically caused by plastic toothbrushes and advocating on the adoption of eco-friendly toothbrushes to reduce the plastic pollution caused by plastic toothbrushes. The project is structured to have two phases that will start from November 2023 to April 2024 and May 2024 to November 2024. The project includes physical meetings with target groups as well as online and social media campaigns OBJECTIVES The objective of the advocacy campaign is to raise awareness of the environmental impact of plastic toothbrushes while encouraging people to make the switch to eco-friendly toothbrushes. Specifically, the objectives are: 1. To educate the public on the harmful effects of plastic toothbrushes on the environment. 2. To promote t...