Skip to main content

SARATANI YA KINYWA

 SARATANI YA KINYWA

Saratani ni ukuaji wa seli za mwili usiodhibitiwa ambao hupelekea kuvamia tishu za jirani na kuziharibu. 
Saratani ya kinywa hutokea kama kidonda au ukuaji wa tishu usiopotea. Saratani ya kinywa hujumuisha saratani ya midomo (lips), ulimi, mashavu, chini ya ulimi, taya ya juu, na  koo. saratani ya kinywa inaweza kuhatarisha maisha isipogundulika na kutibiwa mapema.

Image result for oral cancer Saratani ya chini ya ulimi
Image result for squamous cell carcinoma of the lip Saratani ya mdomo
Image result for squamous cell carcinoma of the cheek Saratani ya ulimi


DALILI ZA SARATANI YA KINYWA.
  • Uvimbe kwenye maeneo mbalimbali ya kinywa
  • Kutokwa na damu katika kinywa kusikokua na sababu
  • Kupata ganzi, kutohisi chochote katika kinywa na maumivu wakati wa kugusa eneo lolote la kinywa, uso au shingo
  • Uwepo wa vidonda kwenye kinywa uso au shingo ambavyo huvuja damu kwa urahisi na kutopona kwa wiki mbili au zaidi.
  • Maumivu ya sikio
  • Kutoweza kula, kuongea na kuchezesha taya au ulimi
  • Kupungua uzito kwa ghafla
Ukiwa na dalili hizi tafadhali onana na Daktari wa kinywa na meno Haraka

NANI YUPO KATIKA HATARI YA KUPATA SARATANI YA KINYWA?

Kwa mujibu wa shirika la Saratani Marekani, wanaume wako katika hatari mara mbili zaidi kuliko wanawake na wanaume wenye umri wa miaka 50 au zaidi wapo kwenye hatari zaidi.

Sababu hatarishi zinazopelekea kupata saratani ya kinywa;
  • Uvutaji wa sigara
  • Ulaji wa ugoro. Hii husababisha hasa saratani ya midomo(lips) na mashavu.
  • Unywaji wa pombe kupindukia
  • Kuwepo na historia ya saratani katika familia
  • Uwepo wa kirusi cha Human Papilloma Virus.
NINI KIFANYIKE KUZUIA SARATANI YA KINYWA?
  • Usivute sigara au kutumia ugoro
  • Hakikisha unakula mlo kamili
  • Fanya maangalizi ya afya ya kinywa na meno mara kwa mara ili kugundua tatizo mapema likiwepo. Asilimia 25% ya saratani huwakuta watu ambao sio watumiaji wa tumbaku au pombe.

Comments

Popular posts from this blog

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika. Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea. Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako. 1. Balehe Mabadiliko ya...

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025

 

PLASTIC FREE SMILES PROJECT 2023-2024

  Plastic Free Smiles project is an environmental and oral health project designed by Dr. Winfred Mgaya under the umbrella of Tanzania Oral Health Foundation. The project aims to raise awareness on the effects of plastic pollution to the environment specifically caused by plastic toothbrushes and advocating on the adoption of eco-friendly toothbrushes to reduce the plastic pollution caused by plastic toothbrushes. The project is structured to have two phases that will start from November 2023 to April 2024 and May 2024 to November 2024. The project includes physical meetings with target groups as well as online and social media campaigns OBJECTIVES The objective of the advocacy campaign is to raise awareness of the environmental impact of plastic toothbrushes while encouraging people to make the switch to eco-friendly toothbrushes. Specifically, the objectives are: 1. To educate the public on the harmful effects of plastic toothbrushes on the environment. 2. To promote t...