Skip to main content

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO


Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika.

Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea.

Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako.

1. Balehe

Mabadiliko ya homoni katika kipindi hiki yanaweza kupelekea magonjwa ya fizi na kuwaacha wasichana wengi kupata vidonda, damu kutoka na uvimbe katika fizi. unahitaji kufanya usafi wa kinywa mara mbili kwa siku kwa kutumia dawa yenye madini ya flouride, kusafisha meno kwa kutumia uzi maalum au floss na kumuona daktari wa kinywa na meno mara kwa mara.

2. Hedhi

Unaweza usihisi mabadiliko yoyote katika kinywa chako siku chache kabla ya hedhi, lakini kama ikitokea kupata vidonda mdomoni, fizi kuvimba na kutoa damu basi sababu kubwa huwa ni mabadiliko ya kiwango cha homoni na huisha pale tu siku za hedhi  zinapokwisha. ikitokea dalili hizo zinaendelea basi kuna sababu nyingine zaidi ya homoni, ni vizuri kumuona daktari wa kinywa na meno kwa msaada zaidi. 

3. Matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango

Matatizo ya fizi ni moja ya athari za matumizi ya vidonge vya uzazi wa mpango ambayo wanawake wengi wamekua wakikumbana nayo. Habari njema ni kwamba sasa dawa nyingi zimepunguzwa homoni na kupelekea kupunguza athari ya matatizo ya fizi kwa kiwango kikubwa. Ni vyema kumjulisha daktari wako wa kinywa na meno kama unatumia dawa za uzazi wa mpango kwa sababu;

  • Kuna baadhi ya dawa ambazo zinaweza kufanya nguvu ya vidonge vya uzazi wa mpango kupungua hivyo basi ni vyema daktari akafahamu ili kuziepuka
  • Ukitolewa jino unakuwa kwenye hatari ya kupata maumivu zaidi kwa tafiti zinavyoonesha, hivyo ni vyema daktari akafahamu ili kuzuia athari hiyo mapema.
4. Ujauzito

Wakati wa ujauzito mwili wako unakua katika hali ya uwepo wa kiwango cha juu cha homoni, baadhi ya wanawake hupata matatizo ya fizi hasa katika kipindi cha miezi minne mpaka sita ya ujauzito, hii upeleke pia fizi kuvimba kwa kiasi kikubwa. Ni vyema kuzingatia sana usafi wa kinywa na kumuona daktari wa kinywa na meno angalau kila mwezi kwa ajili ya usafi wa kinywa na uchunguzi wa kawaida.

5. Kukoma Hedhi (Menopause)
 
Kukoma hedhi ni mabadiliko makubwa katika mwili, maisha na kinywa cha mwanamke. Huambatana na mabadiliko ya ladha, hali ya kuhisi kuungua katika kinywa na kupata ganzi katika meno (sensitivity). Hivi vyote huusiana sana na mabadiliko ya homoni.
Kuna vitu viwili vya kuzingatia sana; mdomo mkavu na kupoteza kwa sehemu ya mfupa wa taya. Mate ndio kisafisha kinywa asilia na hufanya kazi hiyo pale ambapo unakuwa husafishi kinywa kwa mswaki, mate yakianza kupungua na kusababisha mdomo mkavu, huleta hatari ya kutoboka meno. Ongea na daktari kama ukihisi kupata mdomo mkavu, epuka matumizi ya vitu vyenye sukari na caffein, pilipili, chumvi nyingi badala yake utumie vile visivyo na sukari (Sugarfree).
Kupoteza sehemu ya mfupa wa taya hupelekea kupotea kwa meno pia, hii husababishwa kushuka kwa kiwango cha homoni ya oestrogen. Ni vyema kumuona daktari katika kipindi hiki ili kuhakikisha unapata kiwango sahihi cha madini ya calcium na vitamin D, usivute sigara na punguza matumizi ya makubwa ya pombe.
 


Comments

Popular posts from this blog

VINA SABA NA AFYA YA KINYWA NA MENO

       Je vinasaba vinaweza kutabari uwezekano wa kupata magonjwa ya fizi na meno kutoboka? Je, magonjwa ya kutoboka meno na fizi hurithishwa? Jibu kwa sasa ni HAPANA. Magonjwa ya meno kutoboka na fizi yanachangiwa sana na mazingira na mitindo ya maisha na sio vina saba au kurithishwa. Usafi wa kinywa, vitu unavyokula, matumizi ya tumbaku yana mchango mkubwa sana katika kupata magonjwa ya fizi na meno kutoboka. Vifaa vya uchunguzi vinavyotumiwa na daktari pamoja na picha za xray ndivyo husaidia kujua hali ya afya yako ya kinywa kwa sasa na kutabiri hali katika siku za mbeleni. Chukua hatua sasa katika kuzuia magonjwa ya fizi na meno kutoboka kwa kufanya yafuatayo Piga mswaki angalau mara mbili kwa siku Safisha sehemu ya katikati ya meno yako kwa kutumia uzi maalum au floss Kula chakula bora na chenye afya na punguza matumizi ya vyakula vyenye sukari Fanya uchunguzi wa afya ya kinywa angalau mara mbili kwa mwaka

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025