MAJIPU KATIKA KINYWA (DENTAL ABSCESS)
Majipu katika kinywa (dental abscess) ni uvimbe ambao unakua na majimaji ya njano au usaha. Majipu katika kinywa yapo ya aina mbili; majipu yapatikanayo kwenye fizi (periodontal abscess) na majipu yapatikanayo kwenye meno (periapical abcess).
Nini husababisha Majipu katika kinywa?
Majipu hutengenezwa pale ambapo vijidudu au bakteria waliopo mdomoni wanapata mazingira mazuri ya kusababisha maambukizi (infection). Majipu hutengeneza kizuizi sehemu ambayo bakteria wamesababisha maambukizi na kuzuia yasisambae sehemu nyingine ya mwili.
Majipu ya fizi hutokea pale bakteria wanapotengeneza maambukizi kati ya fizi na meno, na hii ni matokeo ya mabaki ya vyakula kukwama sehemu hizo. Majipu ya fizi hutumia muda kujitengeneza na mara nyingi hutokea kwa watu wenye magonjwa ya fizi ya muda mrefu.
Majipu ya meno hutokea kwenye ncha ya mzizi wa jino na hutokea pale mishipa fahamu inapoelekea kufa au imekufa kabisa.
![]() |
| Jipu katika Meno |
Dalili za Majipu katika Kinywa
- Maumivu yenye kupwita
- Uvimbe katika maeneo ya kinywa wenye usaha
- Fizi kuwa nyekundu na kuuma
- Maumivu ya jino wakati wa kula au kukiwa na msukumo katika jino
- Harufu mbaya katika kinywa
- Taste mbaya katika kinywa
Jinsi ya kuzuia majipu katika kinywa.
Majipu katika kinywa yanaweza kuzuiwa kwa kuhakikisha unafanya usafi wa kinywa kila siku na kwa usahihi, kuhakikisha hakuna mabaki ya chakula yanabaki katika meno na zaidi checkup za mara kwa mara kwa Daktari wa Meno.


Comments
Post a Comment