Skip to main content

AFYA NA USAFI WA KINYWA KWA WATOTO

AFYA NA USAFI WA KINYWA KWA WATOTO

Image result for black children

Afya njema ya mtoto ni jukumu la mzazi, afya ya kinywa ni kati ya sehemu muhimu ya afya ya mtoto kwa ujumla. Matunzo ya meno na fizi za mtoto huanza na mzazi mwenyewe. Matunzo mazuri ya meno kwa watoto huwasaidia kuwa na afya njema ya kinywa baadae na hupunguza nafasi ya kupata magonjwa ya kinywa wakiwa wakubwa kwa kuwa wanakuwa wametengenezewa mazingira, uwezo na ufahamu wa jinsi ya kutunza meno na umuhimu wa kufanya hivyo.

Usafi wa Kinywa kwa Watoto Wachanga.
 Image result for african INFANTS
Watoto huzaliwa meno yakiwa tayari yamekwisha tengenezwa lakini huwezi kuyaona kwa sababu yanakua ndani ya fizi. Meno huanza kujitokeza nje ya fizi mtoto akiwa na umri kuanzia miezi 6 lakini ni vizuri kuanza usafi wa kinywa kwa mtoto hata kabla meno hayajaanza kutoka kwani "kwenye fizi safi na zenye afya huja meno safi na yenye afya".

  • Futa fizi za mtoto kwa kitambaa safi kila baada ya kumlisha, hii husaidia kuondoa bakteria wanaosababisha meno kuoza.
  • Pale meno yanapoanza kuota, hakikisha unaanza kumpigisha mswaki kwa kutumia mswaki laini na dawa ya meno yenye flouride kwa kiwango cha watoto.
  • Ondoa chupa ya maziwa pale mtoto anapomaliza kunywa ili kuzuia kuoza kwa meno kunakosabishwa na maziwa, "baby bottle tooth decay".
  • Hakikisha unapanga miadi "appointment" na daktari wa meno pale mtoto anapoanza kuota meno ya kwanza hii husaidia matunzo ya meno na mazoea mazuri ya mtoto katika mazingira ya matibabu ya meno.
Usafi wa Kinywa kwa Watoto Kuanzia miaka Mitatu
 Image result for 3 year old child
Watoto wakiwa wanakua, wanatakiwa kukua na tabia ya usafi na utunzaji wa afya ya kinywa. Watoto huwa na meno yote wakiwa na umri wa miaka 3. Meno haya huitwa meno ya kitoto au "baby teeth". Meno ya kitoto huanza kutoka wakiwa na umri wa miaka 6, na huo ndio muda ambao meno ya kiutu uzima au "permanent teeth" huanza kuota.

Kwa watoto kuanzia miaka mitatu, yafuatayo ni mambo ya kuzingatia;
  •  Hakikisha anapiga mswaki kwa dawa ya meno yenye flouride kwa kiwango cha watoto 
  • Hakikisha anapiga mswaki mara mbili kwa siku, asubuhi na usiku kabla ya kulala
  • Anza mazoea ya kumfundisha kufloss
  • Kuonana na daktari wa meno kila baada ya miezi sita
 
Usafi wa Kinywa kwa Watoto Kuanzia miaka Saba

Image result for 7 year old child
Watoto wanapokua, meno ya utu uzima yanaanza kuota, usafi wa kinywa ni muhimu kwa ajili ya kufanya fizi na meno yawe katika afya njema. Ingawa ni ngumu kufuatilia watoto wakiwa katika umri huu, yafuatayo ni mambo ya kuzingatia ili kudumisha afya zao za kinywa na meno kwa watoto hawa;
  • Watoto katika umri huu wanakua makini muonekano wao, ni vizuri kuwakumbusha kuwa usafi wa meno na kinywa utasaidia kuwafanya waonekane vizuri zaidi.
  • Wakumbushe watoto kupiga mswaki na dawa ya meno yenye flouride mara mbili kwa siku ili kuzuia meno kutoboka
  • Hakikisha wanavaa vifaa vya kulinda meno yao wakiwa wanafanya michezo ili kuzuia meno kuvunjika wanapokua wameanguka au kupata ajali wakiwa michezoni
  • Hakikisha watoto wanaonana na daktari wa meno kila baada ya miezi sita ili kuhakikisha kila kitu kipo sawa.
AFYA NJEMA NA UKUAJI MZURI WA MTOTO HUTEGEMEA LISHE BORA NA MUHIMU ZAIDI AFYA BORA YA KINYWA AMBAYO NDIO SEHEMU CHAKULA HUPITIA. AFYA BORA YA KINYWA NI AFYA BORA YA MWILI MZIMA.

Comments

Popular posts from this blog

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika. Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea. Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako. 1. Balehe Mabadiliko ya...

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025

 

PLASTIC FREE SMILES PROJECT 2023-2024

  Plastic Free Smiles project is an environmental and oral health project designed by Dr. Winfred Mgaya under the umbrella of Tanzania Oral Health Foundation. The project aims to raise awareness on the effects of plastic pollution to the environment specifically caused by plastic toothbrushes and advocating on the adoption of eco-friendly toothbrushes to reduce the plastic pollution caused by plastic toothbrushes. The project is structured to have two phases that will start from November 2023 to April 2024 and May 2024 to November 2024. The project includes physical meetings with target groups as well as online and social media campaigns OBJECTIVES The objective of the advocacy campaign is to raise awareness of the environmental impact of plastic toothbrushes while encouraging people to make the switch to eco-friendly toothbrushes. Specifically, the objectives are: 1. To educate the public on the harmful effects of plastic toothbrushes on the environment. 2. To promote t...