Skip to main content

Posts

Showing posts from March, 2020

TATIZO LA KUSAGA MENO.

TATIZO LA KUSAGA MENO.   Asilimia kubwa ya watu wana tatizo la kusaga meno ambalo kitaalamu linafahamika kama "bruxism". Tatizo hili la kusaga meno huenda sambamba na kukaza kwa taya (jaw clenching) Kuna aina mbili la tatizo hili la kusaga meno au bruxism, sleep/noctunal bruxism ambalo hutokea wakati mtu akiwa amelala na diurnal/awake bruxism ambalo hutokea wakati mtu akiwa macho. Aina zote mbili zina vitu vinavyofanana ambavyo ni kusaga meno na kukaza kwa taya. Ni ngumu kugundua kama una tatizo la kusaga kwa sababu mara nyingi hutokea bila kufahamu lakini kama una hizi dalili basi una tatizo la kusaga meno  Maumivu ya taya na kupungua kwa kufunguka kwa mdomo Meno yaliyosagika na kuvunjika Maumivu ya kichwa Maumivu ya masikio Ingiwa mtu yoyote anaweza akapata tatizo hili ila huwapata sana watu wenye umri kuanzia miaka 20-40 Athari za kusaga meno. Kwanini watu wanasaga meno? Kuna sababu nyingi zinazopelekea watu kusaga meno, lakini inaaminika kuwa sa...

AFYA YA KINYWA NA MENO KWA WAJAWAZITO

AFYA YA KINYWA NA MENO KWA WAJAWAZITO Ujauzito ni kipindi ambacho mwanamke anakua ana mahitaji mengi na mabadiliko mengi katika mwili na baadhi ya mabadiliko hayo yana athari kwa afya ya kinywa na meno kama hakutakua na uangalizi mzuri wa kinywa na meno kwa kipindi cha ujauzito. Moja ya matatizo ya kinywa na meno yanayowapata wajawazito wengi ni tatizo la fizi kuvimba na kutoa damu ambayo kitaalamu inaitwa "pregnancy gingivitis au pregnancy tumour". Tatizo hili husababishwa na kuongezeka kwa kiwango cha homoni iitwayo "progesterone" ambayo huchangia kuongezeka kwa mtirirko wa damu kwenye fizi na kuzifanya ziwe sensitive, kuvimba na rahisi kutoa damu wakati wa kupiga mswaki. Mabadiliko ya kiwango cha homoni hii pia huwapa urahisi bakteria ambao husababisha magonjwa ya fizi kukua na kusababisha magonjwa ya fizi. Tatizo hili la fizi linaweza kutokea muda wowote kuanzia mwezi wa pili mpaka wa nane lakini huwa kwa kasi sana katika kipindi cha pili cha ujauzit...

UMRI NA AFYA YA KINYWA NA MENO

UMRI NA AFYA YA KINYWA NA MENO Umri ukiwa unaongezeka inakua ni muhimu zaidi kuwa muangalifu na afya ya kinywa na meno. Kuna imani potofu kuwa kadiri mtu anavyozeeka ndivyo anavyopoteza meno yake, SI KWELI.  Kama unapiga mswaki vizuri na kuwa muangalifu na afya ya kinywa na meno, meno yako yanaweza kubaki maisha yako yote. Kinywa hubadilika umri ukiwa unaongezeka, mishipa ya fahamu kwenye meno hubadilika na kuwa midogo zaidi na kukufanya kutohisi sana maumivu pale meno yanapotoboka. Kama utakua hufanyi check up ya meno mara kwa mara, hii hufanya matatizo yagundulike yakiwa katika hatua mbaya ambayo mara nyingine inaweza ikashindikana kutibiwa na kupeleke kupoteza meno. Kama unataka kujisikia vizuri, kuwa na fya na muonekano mzuri, utashangazwa na jinsi kinywa chenye afya kinaweza kukubadilisha. Vifuatavyo ni vidokezo vinavyoweza kukusaidia kudumisha na kuboresha afya ya kinywa na meno kwa maisha yako yote. Piga mswaki angalau mara mbili kwa siku kwa mswaki laini na d...

MATATIZO YA TUMBO NA AFYA YA MENO

MATATIZO YA TUMBO NA AFYA YA MENO Matatizo ya tumbo ya mara kwa mara yanawezaz kusababisha kulika kwa tabaka la juu kabisa la meno kwa mchakato ambao kitaalamu unaitwa "tooth erosion". Kulika kwa tabaka hilo la meno husababisha meno kuwa na muonekano mbaya na pia huhatarisha meno kutoboka. Matatizo ya Tumbo yanaathiri vipi Meno? Tumbo hutengeneza tindikali ya asili ambayo husaidia katika umen'genyaji wa chakula. Mara nyingine tindikali hiyo husafiri kwenye njia ya chakula mpaka mdomoni hasa baada ya kula chakula kingi. Kwa kawaida mate yetu huweka usawa wa tindikali hiyo na kila kitu huwa sawa. Lakini kwa wale ambao hupata tatizo la kubeua au kitaalamu huitwa " gastroesophageal reflux ". Hii husababisha tindikali kufika mdomoni mara nyingi sana, tindikali hii huanza kushambulia meno na kuondoa taratibu tabaka la juu kabisa la meno. Tatizo hili huwa linatokea sana wakati unapokua umelala kwa sababu mzunguko wa mate mdomoni huwa mdogo na hivyo kushind...

MATUMIZI YA ANTIBIOTICS KATIKA AFYA YA KINYWA NA MENO

 MATUMIZI YA ANTIBIOTICS KATIKA AFYA YA KINYWA NA MENO   Antibiotics hutolewa pale ambapo kuna maambukizi au ugonjwa unaosababishwa na bakteria. Linapofika suala la maumivu ya jino, antibiotics zinatakiwa kuepukwa isipokua pale ambapo kuna uhitaji sana wa kuzitumia. Kuwa na uelewa kuhusu antibiotics kutasaidia kuweza kuelezea vizuri jinsi ambavyo unajisikia kwa daktari wa meno na kupata jinsi ya kutatua tatizo. Kwa kujua dalili za maumivu ya jino daktari anaweza kujua ni matibabu gani yanafaa kulingana na tatizo. ni Daktari pekee ndiye anayejua ni wakati gani unafaa kutumia antibiotics na upi haufai kulingana na tatizo na maumivu. Antibiotics hutolewa mara nyingi kwa maambukizi au infection ambayo imesambaa na hii huweza kutambulika kama daktari akishakuona na kutambua ukubwa wa tatizo. Dawa ni za kipekee. Hatuwezi kushiriki kutumia mswaki mmoja si ndivyo? Basi ndivyo ilivyo kwenye madawa, dawa inayomsaidia mtu mmoja inaweza isifanye kazi kwa mtu mwingin...

DAWA YA KUSUKUTUA MDOMO

DAWA ZA KUSUKUTUA MDOMO Ingawa sio mbadala wa kupiga mswaki, matumizi ya dawa za kusukutua au mouthwash yanasaidia katika kuimarisha afya ya kinywa na meno. Kwanini tunahitaji kutumia Dawa za Kusukutua Mdomo? Kama ambavyo uzi wa kusafishia meno (dental floss) ufanyavyo, dawa za kusukutua mdomo pia hufika sehemu ambazo mswaki hauwezi kufika na husaidia kupunguza hatari ya kuoza meno na kupata magonjwa ya fizi na pia hufanya kinywa kiwe fresh na kuwa na harufu nzuri. Aina za Dawa za kusukutua Mdomo Dawa za kusukutua mdomo kwa ajili ya tiba (Therapeutic Mouthwash) ; Hizi ni dawa zenye viungo hai (active ingredients) kama flouride ambazo husaidia kuondoa utando juu ya meno, meno kuoza, magonjwa ya fizi na harufu mbaya ya kinywa. Na pia kuna ambazo ni maalumu kwa watu ambao wana matatizo ya kinywa kama vidonda au majeraha ya ajali.                                      ...

TATIZO LA KUKOSA PUMZI NA KUKOROMA WAKATI WA KULALA

TATIZO LA KUKOSA PUMZI  NA KUKOROMA WAKATI WA KULALA Kukosa pumzi wakati wa kulala (sleep apnea) ni tatizo ambalo hutokea wakati upumuaji wa kawaida huingiliwa wakati mtu akiwa usingizini. Kukoroma ni tatizo linalowapata watu wengi wanaopata shida ya ya kupumua wakati wakiwa usingizini ila sio wote wanaokoroma wanapata shida ya kupumua. Kuna aina mbili za kukosa pumzi wakati wa usingizi; Obstructive sleep apnea. Hii ndio ya kawaida na inawapata watu wengi. Hutokea pale njia ya hewa inapokua imezibwa wakati wa usingizi. Matatizo ya kiafya kama uzito uliopitiliza huchangia sana kwenye hili. Central sleep apnea. Hii hutokea pale ambapo ubongo unashindwa  kupeleka taarifa na kuamsha misuli ya upumuaji. Njia za hewa zinakua wazi ila ubongo hushindwa kuamsha misuli. Hii huwapata sana watu waliopooza, wenye saratani ya ubongo na moyo kushindwa kufanya kazi(heart failure). Tatizo la kukosa pumzi usingizini linaweza kumpata mtu yoyote katika umri wowote. Ingawa wan...