Watu wengi wanatokea kusahau kufanya usafi wa kinywa na meno wakiamini kuwa hakuna tatizo litawapata katika kipindi cha mfungo. Kuhakikisha usafi wa kinywa na meno utasaidia kupunguza harufu mbaya ya kinywa na kinywa kuwa kikavu. NINI HUTOKEA UKIWA UMEFUNGA? Kufunga husababisha kuongezeka kwa kampaundi za madini ya sulphur katika kinywa na husababisha harufu mbaya ya kinywa. Watu wengi wanaamini kuwa kufunga husaidia kutibu magonjwa ya fizi, hii sio kweli. Kuongezeka kwa kampaundi za madini ya sulphur huenda sambamba na kupungua kwa mtiririko wa mate katika kinywa ambayo husababisha kutengenezwa kwa matabaka ya uchafu katika meno kitu ambacho moja kwa moja hupelekea matatizo ya fizi na meno kutoboka. JINSI YA KUTUNZA AFYA YA KINYWA NA MENO KIPINDI CHA MFUNGO. Changamoto nyingi za afya ya kinywa na meno huwepo kipindi cha mfungo. Wengi wamezoea harufu mbaya ya kinywa katika kipindi cha mfungo na huwa wanahisi ni jambo la kawaida. Fanya mamb...
ELIMU,USHAURI NA MSAADA KUHUSU AFYA YA KINYWA. MAWASILIANO: PHONE; +255716817627, +255743507651 EMAIL; tanzaniaoralhealthfoundation@gmail.com