Skip to main content

MENO NI NINI? TUFAHAMU ZAIDI KUHUSU MENO, AINA NA KAZI ZAKE

MENO

Meno ni viungo vya mwili vilivyopo kinywani vyenye kazi ya kutafuna yaani kumega chakula kama maandalizi ya kukimeza na kumeng'enya.
Meno hupatikana kwa wanyama wenye uti wa mgongo. Nje ya kutafuna chakula hutumiwa pia kama silaha za kujilinda au kushambulia wanyama wengine. Wanyama kadhaa huwa na meno nje ya mdomo kwa matumizi kama silaha (mfano: tembo) yanayoweza kutumiwa pia kama vifaa vya kuchimba (mfano: nguruwe mwitu).

Kwa binadamu meno hupatika kinywani tu. Kazi kubwa ya meno kwa binadamu ni katika umeng'enyaji wa chakula anachokula na mara chache watu hutumia katika kusaidia kukata vitu mbalimbali kama kutatua kitambaa au kukata kamba au waya ingawa kufanya hivyo kunaweza kuwa na madhara kwa meno. Binadamu ana aina mbalimbali za meno zinazomsadia kula vyakula vya aina mbalimbali kama vile vya mimea na nyama. Kwa kawaida mtu mzima huwa na meno thelathini na mbili. 

Binadamu huwa na aina mbili za meno. Tunazaliwa na mbegu za meno ya utoto yanayobadilishwa wakati wa kubalehe kwa meno ya kudumu. Kwa hiyo kuna wakaa mbili za meno.
Idadi ya meno ya utoto katika wakaa ya kwanza ni 20. Huanza kuota mtoto anapokuwa na umri wa miezi sita na kawaida yote huwa yamekwisha kuota mtoto anapotimiza umri wa miaka miwili.
Idadi ya meno katika wakaa ya pili ni 32. Huanza kuota katika umri wa miaka sita, yakakamilika katika umri wa miaka 18-20. Lakini mwingine huota upesi au hukawia.

                                                                    Meno ya kudumu.
                                                                  Meno ya watoto.



 AINA ZA MENO
Umbo la meno hufuatana na kazi ambayo inayapasa kufanya. Meno yaliyopo katikati ya kila taya huwa na kingo kali za kukatia chakula. Haya huitwa meno ya kukatia au meno ya mbele (incisors). (meno 8 ya kukatia, katika kila taya yapo meno 4).
Meno yanayofuata meno ya kukatia ni machonge (canine teeth). Yapo machonge 4 kwa ujumla; katika kila taya kuna machonge 2. Kazi yao ni kurarua chakula.
Meno yanayofuata machonge huitwa magego madogo (premolars) (jumla ya magego madogo ni 8; na katika kila taya yapo 4); na meno yanayoyafuata hayo huitwa magego (molars) (magego yote ni 12, na katika kila taya kuna magego 6. Magego madogo na magego ni kwa kusagia chakula. Katika meno ya watoto huwa hakuna magego madogo.



 MUUNDO WA JINO
Meno hukaa kwa uthabiti ndani ya vitundu vya mataya. Kila jino lina sehemu mbalimbali. Sehemu ambayo huonekana kinywani ni kichwa cha jino (tajino), na sehemu iliyomo ndani ya taya ni mzizi wa jino.
Sehemu kubwa ya jino ni mfupa laini unaoitwa dentini. Dentini kwenye sehemu ya tajino au kichwa hufunikwa kwa gamba la jino. Kichwa ni cha ufupa mgumu sana wenye rangi nyeupe ya kung’aa unaoitwa enameli ya jino. Kazi yake ni kulinda mfupa laini zaidi ya ndani. Pembe ya shina hulindwa na tabaka aina ya saruji ijulikanayo kwa jina la kitaalamu kama sementi ya jino (ing. cementum).
Katikati hasa ya sementi ya jino na mfupa wa taya kuna utando, ambao unasaidia kukuza jino katika kitundu chake, nao (utando huo) hulingana na ufizi wa meno.
Ndani ya jino kuna uwazi mwenye tishu ya neva na mishipa ya damu. Neva pamoja na mishipa ya damu huingia katika mvungu penye ncha ya kizizi cha jino.


Comments

Popular posts from this blog

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika. Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea. Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako. 1. Balehe Mabadiliko ya...

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025

 

PLASTIC FREE SMILES PROJECT 2023-2024

  Plastic Free Smiles project is an environmental and oral health project designed by Dr. Winfred Mgaya under the umbrella of Tanzania Oral Health Foundation. The project aims to raise awareness on the effects of plastic pollution to the environment specifically caused by plastic toothbrushes and advocating on the adoption of eco-friendly toothbrushes to reduce the plastic pollution caused by plastic toothbrushes. The project is structured to have two phases that will start from November 2023 to April 2024 and May 2024 to November 2024. The project includes physical meetings with target groups as well as online and social media campaigns OBJECTIVES The objective of the advocacy campaign is to raise awareness of the environmental impact of plastic toothbrushes while encouraging people to make the switch to eco-friendly toothbrushes. Specifically, the objectives are: 1. To educate the public on the harmful effects of plastic toothbrushes on the environment. 2. To promote t...