Skip to main content

MAGEGO YA MWISHO - (WISDOM TEETH)

       What are wisdom teeth, and should you have them removed?
Magego ya mwisho au wisdom teeth ni meno ya mwisho kabisa kuota katika mdomo na huota kati ya miaka 17 mpaka 25. Meno haya huwa  mawili kwa kila taya  moja kila upande wa taya na kufanya jumla yake iwe manne. Sio watu wote huota haya magego ya mwisho na hata kam yakiota kwa watu wengi huwa hayajakaa katika mstari kama meno mengine lakini kwa wachache huwa yanaota vizuri kabisa.

Mara nyingi magego ya mwisho huotea ndani ya taya na hayatoki nje na hata kama yakitoka huota vibaya na kusababisha kuoza na hata magonjwa ya fizi hii husababishwa na kuwepo kwa fizi juu ya meno haya ambayo huifadhi vyakula na kusababisha infection na maumivu.

Kwanini magego ya mwisho huota vibaya?

Magego ya mwisho huota vibaya kwasababu hayapati nafasi ya kuota kwa kawaida. Magego ya mwisho huota kati ya miaka 17 mpaka 25, umri ambao mdomo tayari unakua na meno mengi hivyo basi kukosa nafasi ya kuota vizuri na kuishia kuota katika hali ambayo sio ya kawaida (impacted).

Matatizo yanayoweza kuletwa na Magego ya mwisho ambayo hayajaota vizuri.
  • Uharibifu kwa meno mengine
  • Kutengenezwa kwa kimfuko chenye maji au CYST ambacho kinaweza kuleta athari kwa mfupa na mishipa ya fahamu
  • Meno kuoza
  • Magonjwa ya fizi
Mara nyingi picha ya xray huchukuliwa kuangalia jinsi magego haya ya mwisho yalivyokaa.

Je kuna ulazima wa kuyatoa magego ya mwisho?

Kwa magego ya mwisho ambayo hayajaota vizuri, ni vizuri kuyatoa ili kuepusha matatizo yanayoweza kutokea baadae kutokana na ukaaji wa magego hayo. Kulingana na sehemu jino lilipo na lilivyoota, magego ya mwisho yanaweza kutolewa katika kliniki ya meno au katika chumba cha upasuaji.


Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

HOMONI NA AFYA YA KINYWA NA MENO - VITU AMBAVYO KILA MWANAMKE ANAPASWA KUJUA

 HOMONI ZA KIKE NA AFYA YA KINYWA NA MENO Uzito. Hisia, Mahitaji ya kimwili(sex drive). Afya ya kinywa na meno. Ni vitu ambavyo vinaweza kufanya afya yako ya mwili ikabadilika. Utashangazwa kujua jinsi mabadiliko ya homoni zako yanaweza kukufanya uwe katika hatari ya kupata magonjwa ya fizi. Sababu ni hii. Uwepo wa homoni nyingi za kike katika mwili wako unasababisha damu nyingi kutiririka katika fizi zako na kuzifanya ziwe sensitive na kuoverreact kwakitu chochote kitakachozikera(irritate). Wanawake wapo sensitive na uwepo wa uchafu katika meno yao pale ambapo homoni zao katika mwili zipo juu, hii  husababisha fizi kuvimba na kutoka damu na kama zisipotibiwa hupelekea kupoteza mfupa unaoshikilia meno na kupelekea meno kupotea. Homoni ni maisha na ni kitu kisichoepukika ila magonjwa ya fizi yanaweza kuzuiwa na kutibika katika hatua zake za mwanzo. Sasa nini kifanyike? Anza kwa kuwa makini na afya ya kinywa chako katika vipindi vitano katika maisha yako. 1. Balehe Mabadiliko ya...

UJUMBE SIKU YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI 2025

 

PLASTIC FREE SMILES PROJECT 2023-2024

  Plastic Free Smiles project is an environmental and oral health project designed by Dr. Winfred Mgaya under the umbrella of Tanzania Oral Health Foundation. The project aims to raise awareness on the effects of plastic pollution to the environment specifically caused by plastic toothbrushes and advocating on the adoption of eco-friendly toothbrushes to reduce the plastic pollution caused by plastic toothbrushes. The project is structured to have two phases that will start from November 2023 to April 2024 and May 2024 to November 2024. The project includes physical meetings with target groups as well as online and social media campaigns OBJECTIVES The objective of the advocacy campaign is to raise awareness of the environmental impact of plastic toothbrushes while encouraging people to make the switch to eco-friendly toothbrushes. Specifically, the objectives are: 1. To educate the public on the harmful effects of plastic toothbrushes on the environment. 2. To promote t...