Kupiga mswaki kwa usahihi ndio njia ambayo inaweza kukufanya uwe na tabasamu zuri na meno yenye mng'ao. Lakini je unawaza kufanya meno yako yawe meupe zaidi? Basi ni vizuri ukajua ukweli kuhusu matibabu haya. Nitaelezea kwa kujibu maswali ambayo huwa yanaulizwa sana kuhusu kufanya meno yawe meupe.
Kwanini Meno yanabadilika rangi?
Kwa muda meno yako yanaweza kubadilika kutoka rangi nyeupe kwenda kwenye rangi iliyofifia kutokana na sababu tofauti ambazo ni;
Matibabu ya kufanya meno kuwa meupe hutumia dawa ambazo zina kemikali salama ambazo hufanya meno yawe meupe. Kemikali hizi ni hydrogen peroxide na carbamide peroxide.
Whitening inafanya kazi kwenye meno ya aina yote?
HAPANA. Hii ni sababu pia inayoshauriwa kuongea na daktari wa meno kabla ya kufanya utaratibu huu wa kung'arisha meno. Whitening haifanyi kazi kwenye meno yote yaliyobadilika rangi inategemea na sababu ya kubadilika rangi. Meno yaliyobadilika rangi kwa sababu ya ajali au madawa hayawezi kufanyiwa whitening kabisa.
Ni njia zipi naweza tumia kufanya whitening?
Ni vyema ukaongea na daktari wako wa meno kuhusu kuwhiten meno yako na machaguo yaliyopo ila kuna njia kuu nne ambazo zinatumika kufanya meno yawe meupe nazo ni;


Nini athari za whitening?
Baadhi ya watu ambao wametumia bidhaa za kung'arisha meno wamepata athari ya meno kuwa na ganzi na pia kutumia bidhaa hizi kwa muda mrefu husbabisha kupungua kwa tabaka la juu la meno.
Ni vyema kuongea na daktari wako ili kujua njia sahihi na matumizi sahii ya bidhaa za kung'arisha meno
Kwanini Meno yanabadilika rangi?
Kwa muda meno yako yanaweza kubadilika kutoka rangi nyeupe kwenda kwenye rangi iliyofifia kutokana na sababu tofauti ambazo ni;
- Vyakula na vinywaji; Kahawa, chai na mvinyo mwekundu ni vinywaji ambavyo vinaleta sana kubadilika kwa rangi ya meno. Vinywaji hivi vina rangi ambayo huganda kwenye tabaka la nje la meno.
- Matumizi ya tumbaku na sigara; Vitu viwili vilivyopo kwenye sigara ndivyo hufanya rangi ya meno ibadilike navyo ni lami na nicotine. Lami ni nyeusi kwa asili lakini nicotine hubadilika rangi inapochanganyika na hewa ya oxygen na kuwa njano ambayo huonekana sana kwenye meno ya wavutaji wa sigara.
- Umri; Chini ya tabaka gumu kabisa la meno kuna tabaka ambalo ni laini kidogo liitwalo dentine, umri unavyosogea tabaka gumu la juu hupungua na hivyo kupelekea tabaka la dentine kuonekena ambalo lina rangi ya unjano hii ndio sababu wazee wana meno ambayo ni rangi ya njano kidogo.
- Madawa. Kuna baadhi ya madawa ambayo hutumika kwa matibabu tofauti husababisha rangi ya meno kubadilika na pia matibabu ya mionzi.
Matibabu ya kufanya meno kuwa meupe hutumia dawa ambazo zina kemikali salama ambazo hufanya meno yawe meupe. Kemikali hizi ni hydrogen peroxide na carbamide peroxide.
Whitening inafanya kazi kwenye meno ya aina yote?
HAPANA. Hii ni sababu pia inayoshauriwa kuongea na daktari wa meno kabla ya kufanya utaratibu huu wa kung'arisha meno. Whitening haifanyi kazi kwenye meno yote yaliyobadilika rangi inategemea na sababu ya kubadilika rangi. Meno yaliyobadilika rangi kwa sababu ya ajali au madawa hayawezi kufanyiwa whitening kabisa.
Ni njia zipi naweza tumia kufanya whitening?
Ni vyema ukaongea na daktari wako wa meno kuhusu kuwhiten meno yako na machaguo yaliyopo ila kuna njia kuu nne ambazo zinatumika kufanya meno yawe meupe nazo ni;
- Dawa za meno zinazotumika kung'arisha meno. Dawa hizi huwa na kitu ndani yake ambacho husaidia kufanya meno yawe meupe. Ni vizuri kuzifahamu kabla ya kuzitumia kuepuka athari.

- Matibabu ya daktari. Njia hii hutumia dawa maalumu ambayo ina muongozo wa kuitumia na hufanyika katika kliniki ya meno na hufanywa na daktari.

- Dawa za kutumia nyumbani. Dawa hizi hutolewa kwa maelekezo ya daktari ila hutumika nyumbani ukiwa unafuatiliwa kwa ukaribu na daktari na huachwa pale tu weupe wa meno unapoonekana

Baadhi ya watu ambao wametumia bidhaa za kung'arisha meno wamepata athari ya meno kuwa na ganzi na pia kutumia bidhaa hizi kwa muda mrefu husbabisha kupungua kwa tabaka la juu la meno.
Ni vyema kuongea na daktari wako ili kujua njia sahihi na matumizi sahii ya bidhaa za kung'arisha meno
🤝
ReplyDelete