Je vinasaba vinaweza kutabari uwezekano wa kupata magonjwa ya fizi na meno kutoboka? Je, magonjwa ya kutoboka meno na fizi hurithishwa? Jibu kwa sasa ni HAPANA. Magonjwa ya meno kutoboka na fizi yanachangiwa sana na mazingira na mitindo ya maisha na sio vina saba au kurithishwa. Usafi wa kinywa, vitu unavyokula, matumizi ya tumbaku yana mchango mkubwa sana katika kupata magonjwa ya fizi na meno kutoboka. Vifaa vya uchunguzi vinavyotumiwa na daktari pamoja na picha za xray ndivyo husaidia kujua hali ya afya yako ya kinywa kwa sasa na kutabiri hali katika siku za mbeleni. Chukua hatua sasa katika kuzuia magonjwa ya fizi na meno kutoboka kwa kufanya yafuatayo Piga mswaki angalau mara mbili kwa siku Safisha sehemu ya katikati ya meno yako kwa kutumia uzi maalum au floss Kula chakula bora na chenye afya na punguza matumizi ya vyakula vyenye sukari Fanya uchunguzi wa afya ya kinywa angalau mara mbili kwa mwaka
ELIMU,USHAURI NA MSAADA KUHUSU AFYA YA KINYWA. MAWASILIANO: PHONE; +255716817627, +255743507651 EMAIL; tanzaniaoralhealthfoundation@gmail.com