Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2020

KUNG'ARISHA MENO (TEETH WHITENING) - VITU UNAVYOPASWA KUJUA

Kupiga mswaki kwa usahihi ndio njia ambayo inaweza kukufanya uwe na tabasamu zuri na meno yenye mng'ao. Lakini je unawaza kufanya meno yako yawe meupe zaidi? Basi ni vizuri ukajua ukweli kuhusu matibabu haya. Nitaelezea kwa kujibu maswali ambayo huwa yanaulizwa sana kuhusu kufanya meno yawe meupe. Kwanini Meno yanabadilika rangi? Kwa muda meno yako yanaweza kubadilika kutoka rangi nyeupe kwenda kwenye rangi iliyofifia kutokana na sababu tofauti ambazo ni; Vyakula na vinywaji; Kahawa, chai na mvinyo mwekundu ni vinywaji ambavyo vinaleta sana kubadilika kwa rangi ya meno. Vinywaji hivi vina rangi ambayo huganda kwenye tabaka la nje la meno. Matumizi ya tumbaku na sigara; Vitu viwili vilivyopo kwenye sigara ndivyo hufanya rangi ya meno ibadilike navyo ni lami na nicotine. Lami ni nyeusi kwa asili lakini nicotine hubadilika rangi inapochanganyika na hewa ya oxygen na kuwa njano ambayo huonekana sana kwenye meno ya wavutaji wa sigara. Umri; Chini ya tabaka gumu kabisa la meno ku...

UKWELI KUHUSU NJIA ZA ASILI ZINAZOTUMIKA KUNG'ARISHA MENO

Linapofika suala la kufanya meno yawe meupe, kuna njia nyingi ambazo zimekua zikiwekwa kwenye mitandao ya jamii na hata magazeti. Watu wengi wakiulizwa ni njia gani wanahisi wataweza kuifanya tabasamu lao liwe zuri zaidi majibu yao ni kwa kufanya meno yawe meupe zaidi. Tabasamu lenye afya huja katika njia tofauti, ingawa inatamanisha kufikiri kwamba vitu tulivyonavyo jikoni vinaweza vikawa ufumbuzi wa tabasamu zuri. Njia kuwa ya asili haimaanishi ni njia ya kiafya. Njia za kiasili zinaweza kusababisha matatizo makubwa kuliko faida ambayo unaiwaza kuipata. Zifuatazo ni baadhi ya njia ambazo watu huhisi ni sahihi lakini kiafya zina madhara katika meno yako. MAGADI (BAKING SODA) Watu hutumia mchanganyo wa magadi na tindikali zitokanazo na matunda kama machungwa na mananasi.                        Ukweli ni kwamba, kula matunda kiafya ni vizuri lakini mchanganyo wa magadi na ...